Abidjan

Abidjan ndio mji mkubwa zaidi nchini Cote d'Ivoire pia ni bandari kuu ya nchi kwenye Ghuba ya Guinea ya bahari ya Atlantiki. Abidjan haiko baharini moja kwa moja lakini kwenye wangwa ya Ebrie inayotengwa na bahari kwa kanda nyembamba ya mchanga.

Ilikuwa pia mji mkuu rasmi tangu mwaka 1934 hadi 1983. Kwa sasa imetambulika rasmi kama mji mkuu kiuchumi na bado ofisi nyingi za serikali na balozi za nchi nyingine ziko Abidjan.

Abidjan imekua haraka kuanzia wakazi 65,000 mwaka 1950 hadi 4,707,000 mwaka 2014.[1]

Kuna viwanda vya ngozi, nguo, vyakula na mafuta.

Usafiri jijini Abidjan.
Eneo la Plateau na wangwa wakati wa usiku.
  1. Statoids, Departments (Wilaya) of Cote d'Ivoire (2000) (Kiingereza)

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne