Abimeleki

Abimeleki alivyochorwa na Guillaume Rouillé katika Promptuarii Iconum Insigniorum.
Mchoro wa Gustave Doré, Kifo cha Abimeleki.

Abimeleki (kwa Kiebrania אֲבִימָלֶךְ, ’Ǎḇîmeleḵ[1]) mwana wa Gideoni [2] alikuwa mfalme wa Shekemu kwa muda mfupi wakati wa Waamuzi wa Biblia[3].

Kadiri ya Waamuzi 9:1-5 alipata ufalme kwa kuua ndugu zake wote 70, isipokuwa Yothamu aliyenusurika. Huyo alitoa hotuba yenye mfano dhidi ya Abimeleki na watu wa Shekemu waliomuunga mkono (Waamuzi 9:7-15).

Baada ya vita mbalimbali, alijeruhiwa vibaya na mwanamke aliyemrushia kutoka juu jiwe kubwa kichwani. Hapo aliagiza msaidizi wake ammalize kwa upanga.

  1. His name can best be interpreted as "my father is king"
  2. Waamuzi 8:31
  3. chapter nine

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne