Afrika ya Kiroma

Sarafu ya Kaisari Hadrian iliyotolewa kwa heshima ya jimbo la Africa. Mtu ambaye ni mfano wa Africa avaa kofia ya tembo.
Dola la Roma mnamo 120 BK; jimbo la Afrika lina rangi nyekundu.
Ramani ya jimbo mnamo 125 BK.

Afrika hapo awali lilikuwa jina la jimbo la Dola la Roma katika mwambao wa Mediteranea huko Afrika Kaskazini miaka 146 KK - 698 BK. Eneo lake lilikuwa takriban Tunisia ya kaskazini pamoja na pwani ya Libya ya magharibi na Algeria ya mashariki.

Jimbo lilikuwa maarufu kama "ghala ya ngano" ya Roma.

Watu wa Afrika ya Kaskazini kiasili walikuwa hasa Waberber.

Miji muhimu ilikuwa Karthago na Leptis Magna.

Bara la Afrika limepokea jina lake kutoka jimbo hili. Waarabu waliendelea kutawala eneo lake kwa jina la jimbo la Ifriqiya ambalo ni matamshi yao ya "Afrika".


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne