Aktiki (pia: Aktika) ni sehemu ya kaskazini kabisa ya dunia yetu, ikijumlisha nchi na bahari inayozunguka ncha ya kaskazini. Sehemu za kaskazini za Urusi, Alaska (Marekani), Kanada, Greenland (Udani), Skandinavia (Norwei, Uswidi na Ufini) pamoja na bahari ya Aktiki huhesabiwa katika Aktiki.
Zote huwa na hali ya hewa baridi mwaka wote.
Upande wa kusini wa dunia kuna eneo linalolingana na hilo ambalo huitwa Antaktiki.