Antusa wa Konstantinopoli (pia: Antusa Kijana; Konstantinopoli, leo nchini Uturuki, 750 au 757 – 801 au 808) alikuwa binti Konstantino V, kaisari aliyekataza picha takatifu.
Alipofariki, Antusa alijitosa kuhudumia maskini, kukomboa watumwa, kujenga makanisa na monasteri. Alipofariki hata pacha wake (Kaisari Leo VI) aliyetawala miaka 5, Antusa alikataa kuongoza dola kwa niaba ya mtoto wa Leo, Konstantino VI, akawa mmonaki kwa mikono ya Patriarki Tarasi[1].
Tangu zamani anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu bikira.