Ari (kutoka neno la Kiarabu; kwa Kiingereza: zeal) ni adili linalompasa mtu katika utumishi wa Mungu. Ari kwa utukufu wake na kwa wokovu wa watu ni ari moja, ni umotomoto wa upendo uleule unaotakiwa kuwepo hata katika ukavu na majaribu ya kila aina; pengine huo umotomoto wa utashi una juhudi na stahili kadiri mtu asivyouhisi.