Babeli

Sehemu ya geti la Ishtar huko Babeli.
Mnara wa Babeli ulichorwa mara nyingi na wasanii kama katika picha hii ya Pieter Brueghel Mzee.

Babeli ulikuwa mji wa kale katika Mesopotamia, muhimu kwa karne nyingi kama mji mkuu wa milki zilizotawala maeneo makubwa ya Mashariki ya Kati.

Inatajwa mara nyingi katika Biblia, hasa kwa jina la Babuloni.

Maghofu yake hupatikana karibu na mji wa kisasa wa Al Hillah (Irak) kando ya mto Frati km 90 kusini kwa Baghdad.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne