Bahari Kuu (ing. w:ocean) ni jina linalotumika kutaja jumla ya maeneo makubwa ya maji ya chumvi duniani yanayopakana na kufuatana kama gimba moja. Kwa maana hii bahari kuu inafunika zaidi ya theluthi mbili za uso wa dunia.
Bahari Kuu imegawiwa na ardhi ya mabara kwenye nusutufe ya kaskazini ya dunia lakini sehemu zake zinaungana kwenye nusutufe ya kusini.