Bandari asilia

Vidaka vinafaa kama bandari asilia
Bandari ya Dar es Salaam kwenye mdomo pana wa mto Kurasini unaoingia barani kwa kilomita kadhaa

Bandari asilia ni mahali panapofaa kama kituo cha meli kutokana na tabia zake za kiasili. Nafasi ya aina hii inapatikana mara nyingi katika kidaka, kwenye hori au mdomoni wa mto penye kinga dhidi ya upepo na hasa mawimbi ya bahari. Tabia nyingine inayohitajika ni kina cha maji kinacholingana na mahitaji ya meli zinazotumia bandari.

Sharti hili la kina lamaanisha ya kwamba bandari asilia inaweza kuonekana haitoshi tena kwa mahitaji ya meli zilizokuwa kubwa zaidi.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne