Benedikto wa Nursia

Benedikto wa Nursia alivyochorwa na Beato Angelico.
Benedikto wa Nursia alivyochorwa na Giovanni Bellini.

Benedikto wa Nursia (480-547) alikuwa mmonaki wa Italia aliyeandika kanuni ya utawa iliyoenea katika monasteri nyingi za Kanisa la Kilatini na hata nje yake. Wanaoifuata wanaitwa Wabenedikto[1].

Anaheshimiwa tangu zamani kama mtakatifu abati.

Wabenedikto wanaadhimisha sikukuu yake tarehe aliyofariki dunia, lakini kalenda ya Kanisa la Roma inaiadhimisha tarehe 11 Julai[2] tangu Papa Paulo VI alipomtangaza msimamizi mkuu wa Ulaya tarehe 24 Oktoba 1964. Waorthodoksi wanamuadhimisha tarehe 14 Machi.

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/21200
  2. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne