Benedikto wa Nursia (480-547) alikuwa mmonaki wa Italia aliyeandika kanuni ya utawa iliyoenea katika monasteri nyingi za Kanisa la Kilatini na hata nje yake. Wanaoifuata wanaitwa Wabenedikto[1].
Anaheshimiwa tangu zamani kama mtakatifu abati.
Wabenedikto wanaadhimisha sikukuu yake tarehe aliyofariki dunia, lakini kalenda ya Kanisa la Roma inaiadhimisha tarehe 11 Julai[2] tangu Papa Paulo VI alipomtangaza msimamizi mkuu wa Ulaya tarehe 24 Oktoba 1964. Waorthodoksi wanamuadhimisha tarehe 14 Machi.