Brazzaville

Brazzaville.
Kinshasa, Brazzaville na mto Kongo.

Brazzaville ni mji mkuu wa Jamhuri ya Kongo. Una wakazi 2,308,000 (mwaka 2019) ambao ni sawa na 40% ya wananchi wote.

Uko kando ya mto Kongo ukitazamana na mji wa Kinshasa ng'ambo ya mto.

Brazzaville una bandari kwenye mto Kongo na mwanzo wa reli kuelekea pwani.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne