Bunzi-karatasi | ||||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Bunzi-karatasi (Belonogaster juncea) kwenye sega lake
| ||||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||
| ||||||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||||||
Jenasi 26, 4 katika Afrika ya Mashariki:
|
Bunzi-karatasi (kutoka Kiing. paper wasps) ni nyigu wakubwa na warefu wenye kiuno chembamba na mara nyingi kirefu sana. Ni wana wa nusufamilia Polistinae katika familia Vespidae ya order Hymenoptera. Hujenga masega yao kwa aina ya karatasi wanayotengeneza kwa kutafuna fumwele za mbao na kuchanganya na mate yao. Wanatokea duniani kote isipokuwa Antakitiki. Kuna spishi takriban 1100 ambapo 48 zinatokea Afrika ya Mashariki.