Bunzi-karatasi

Bunzi-karatasi
Bunzi-karatasi (Belonogaster juncea) kwenye sega lake
Bunzi-karatasi (Belonogaster juncea) kwenye sega lake
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye miguu yenye viungo)
Nusufaila: Hexapoda (Wanyama wenye miguu sita)
Ngeli: Insecta (Wadudu)
Ngeli ya chini: Pterygota (Wadudu wenye mabawa)
Oda: Hymenoptera (Wadudu wenye mabawa mangavu)
Nusuoda: Apocrita (Hymenoptera wenye kiuno chembamba)
Familia ya juu: Vespoidea
Familia: Vespidae
Latreille, 1802
Ngazi za chini

Jenasi 26, 4 katika Afrika ya Mashariki:

Bunzi-karatasi (kutoka Kiing. paper wasps) ni nyigu wakubwa na warefu wenye kiuno chembamba na mara nyingi kirefu sana. Ni wana wa nusufamilia Polistinae katika familia Vespidae ya order Hymenoptera. Hujenga masega yao kwa aina ya karatasi wanayotengeneza kwa kutafuna fumwele za mbao na kuchanganya na mate yao. Wanatokea duniani kote isipokuwa Antakitiki. Kuna spishi takriban 1100 ambapo 48 zinatokea Afrika ya Mashariki.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne