Bwawa

Bwawa la Ndakaini, Thika.
Maji ya Ndakaini hutumiwa na wakazi wa Jiji la Nairobi.
Bwawa la Haweswater linalosambaza maji Manchester, Uingereza.
Bwawa la kuzalisha umeme.

Bwawa ni mkusanyiko wa maji mengi. Ni dogo kuliko ziwa na mara nyingi huwa limetengenezwa na binadamu. Kwa kawaida, maji huzuiwa kutumia lambo katika bonde la mto au katika ardhi iliyochimbwa, ili kuhifadhi maji. Ingawa kuna mabwawa yaliyo na neno 'ziwa' katika jina, tofauti kuu ni kuwa bwawa hutengenezwa na binadamu[1].

  1. Susanna Scott. "How Lakes Differ - Lake Scientist". Iliwekwa mnamo 2018-04-17.

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne