Carlos Spano (Málaga, Hispania, 1773 - Talca, Chile, 4 Machi 1814) alikuwa askari wa jeshi la Hispania, pia alikuwa shujaa wa vita vya uhuru wa Chile.
Spano alianza kazi yake ya kijeshi mwaka 1786 kama askari katika Jeshi la Hispania, na kupigana katika kampeni za Ceuta (Spanish Morocco) na Aragon (dhidi ya Ufaransa). Mnamo mwaka 1787 Spano alinuliwa na Luteni wa Dragones de la Frontera. Spano alimuoa María de las Nieves Ceballos.
Spano aliunga mkono upande wa wazalendo kwenye Vita vya Uhuru wa Chile, na mwaka 1813 alipandishwa cheo na kuwa mmoja wa kikosi. Novemba 27, 1813, alipandishwa cheo na kuwa Kanali na kupewa jina la Kamanda Mkuu badala ya Juan José Carrera.