Chuo Kikuu ni taasisi ya elimu ya ngazi ya juu ambako wanafunzi wanafundishwa na wataalamu wa fani mbalimbali ambao hufundisha pamoja na kuendesha uchunguzi wa elimu mpya.
Wanafunzi husoma kwenye chuo kikuu kwa shabaha ya kupata elimu hadi kupita mitihani ya shahada au digrii kama vile ya bachelor (ya kwanza), ya uzamili (master) (ya pili) na ya uzamivu, PhD (ya tatu).