Waamuzi 12 na wengineo |
---|
Debora (kwa Kiebrania דְּבוֹרָה|Dvora|Dəḇôrā, yaani Nyuki), mke wa Lapidothi, alikuwa nabii na mwamuzi wa taifa la Israeli katika karne ya 12 KK.
Mwanamke jasiri, aliweza kufanya mambo mengi makubwa katika historia ya wokovu kama inavyoelezwa na Biblia katika kitabu cha Waamuzi, sura 4-5.
Kwa miaka 40 hivi (kama 1160 KK-1121 KK) aliamua Waisraeli chini ya mtende kati ya Rama na Beteli.
Aliongoza pia jeshi la makabila kadhaa ya Israeli ya Kaskazini dhidi ya Yabin, mfalme mmojawapo wa Kanaani, mwenye makao makuu huko Hazor.
Wimbo wa Debora, unaoshangilia ushindi wake katika sura ya 5, ni shairi linalohesabiwa kati ya maandishi ya zamani zaidi ya Kiebrania, ukikadiriwa kuwa uliandikwa katika karne ya 12 KK.[1]