Dikteta

Benito Mussolini (kushoto) na Adolf Hitler (kullia) walikuwa madikteta wa Italia na Ujerumani katika karne ya 20.


Dikteta (kutoka Lat. dictator yaani mwenye kutoa amri kama imla) ni neno la kumtaja mtawala asiyebanwa na sheria na kutumia nguvu ya dola kuendeleza utawala wake na kutokubali upinzani dhidi yake. Pale ambako mtu au kundi la watu hutawala kwa mbinu huu hali ya kisiasa huitwa udikteta. Mfalme anayeweza kuwa na madaraka yaleyale haitwi dikteta.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne