Gaius Aurelius Valerius Diocletianus (takriban 245 – takriban 312) alikuwa Kaizari wa Dola la Roma kuanzia 20 Novemba 284 hadi 1 Mei 305 alipojiuzulu. Alimfuata Numerian.
Kwanza alitawala dola zima, lakini 1 Machi 286 alimteua Maximian kutawala sehemu za Magharibi.
Ni maarufu kwa kuendesha dhuluma kali zaidi ya serikali ya Dola la Roma dhidi ya Wakristo.