Jiji la Dodoma | |
Majiranukta: 6°10′23″S 35°44′31″E / 6.17306°S 35.74194°E | |
Nchi | Tanzania |
---|---|
Mkoa | Mkoa wa Dodoma |
Halmashauri | Halmashauri ya jiji la Dodoma |
Kata | 41 |
Mitaa | 222 |
Serikali[1] | |
- Aina ya serikali | Halmashauri ya jiji |
- Mstahiki Meya | Davis G. Mwamfupe |
- Mkurugenzi wa Jiji | Joseph C. Mafuru |
Idadi ya wakazi (2022)https://www.nbs.go.tz | |
- Wakazi kwa ujumla | 765,179 |
EAT | (UTC+3) |
Msimbo wa posta | 411xx |
Kodi ya simu | 026 |
Tovuti: Halmashauri ya Jiji la Dodoma |
Dodoma ni mji mkuu wa Tanzania na pia ni Jiji.
Ilitangazwa kuwa mji mkuu wa Tanzania mwaka 1973, lakini mnamo tarehe 26 Aprili 2018 katika maadhimisho ya miaka 54 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awamu ya tano John Magufuli aliupandisha hadhi na kutangaza rasmi kuwa Dodoma ni Jiji.[2][3] [4][5][6] Ofisi kuu za wizara na taasisi nyingi za serikali hatimaye zilihamia Dodoma katika miaka 2016 - 2019.[7][8]
Jiji hili pia ni makao makuu ya Mkoa wa Dodoma na eneo lake linahesabiwa kama Wilaya ya Dodoma yenye postikodi namba 41100[9].
Eneo la mji liko mita 1135 juu ya usawa wa bahari UB. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, mji wa Dodoma ulikuwa na wakazi wapatao 410,956 waishio humo.[10]: 17 Mwaka 2022 walihesabiwa 765,179 [11].
<ref>
tag; no text was provided for refs named Dodoma
<ref>
tag; no text was provided for refs named Sensa_2012