Dola Huru la Oranje (Ing.: Orange Free State; Afr.: Oranje-Vrystaat) lilikuwa jamhuri ya makaburu katika Afrika Kusini wakati wa nusu ya pili ya karne ya 19 iliyoundwa na mavoortrekker. Baadaye ilikuwa koloni ya Uingereza na jimbo la Afrika Kusini, tangu 1995 kwa jina "Free State Province" (jimbo la Dola Huru).
Jina la jamhuri lilichaguliwa kutokana na Mto Oranje uliokuwa mpaka wake.