Elimu ya visasili (au mithiolojia, Kiing. mythology, kutoka neno la Kigiriki μυθολογία, mithologia, linaloundwa na μῦθος, mithos, "kisasili" na λογία, logia, "elimu") inahusu utafiti juu ya visasili vya makabila mbalimbali ili kuelewa utamaduni wao.
Jinsi visasili vilivyoanza haijulikani vizuri, lakini vimekuwa vimechunguzwa tangu kale, kwa mfano huko China na Ugiriki wa Kale.
Juhudi kubwa zaidi za kuzilinganisha zilifanywa kuanzia karne ya 19 kwa mitazamo tofauti, chanya au hasi.