Eoni wa Arles

Eoni wa Arles (Chalon-sur-Saône, karne ya 5 BK - Arles, 17 Agosti 502) alikuwa askofu wa mji huo (leo nchini Ufaransa) kuanzia mwaka 485 hadi kifo chake .

Alilinda Kanisa lake dhidi ya uzushi wa Pelaji akapendekeza kwa waumini wake wamfanye mwandamizi wake Sesari[1], ambaye mwenyewe alikuwa amempa upadirisho [2].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 18 Agosti[3].

  1. William E. Klingshirn - Caesarius of Arles : The Making of a Christian Community in Late Antique Gaul, p. 84 e segg.
  2. http://www.santiebeati.it/dettaglio/66530
  3. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne