Farakano la Kanisa la Magharibi

Ramani ikionyesha nchi zilizounga mkono Papa wa Avignon (nyekundu) au Papa wa Roma (buluu) wakati wa farakano la Magharibi; baadaye Mtaguso wa Pisa (1409) ulisababisha mlolongo wa tatu wa waliojidai kuwa Papa halisi.

Farakano la Kanisa la Magharibi lilitokea ndani ya Kanisa Katoliki katika miaka 1378-1418.

Makardinali wenye jukumu la kumchagua Papa walichagua wawili, mmoja baada ya mwingine, na hivyo kusababisha isieleweke yupi ana haki ya kuongoza.

Siasa ilijiingiza na kudumisha fujo kubwa, ingawa si kuhusu mafundisho ya imani, mpaka Mtaguso wa Konstanz (14141418) ulipotoa suluhisho.

Hata hivyo ilibaki athari mbaya juu ya mamlaka ya Mapapa waliofuata.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne