Fransisko Serrano

Wafiadini Wakatoliki wa China.

Fransisko Serrano, O.P. (Hueneja, 4 Desemba 1695Fuzhou, 25 Oktoba 1748) alikuwa askofu mteule kutoka Hispania aliyefanya umisionari barani Asia akauawa nchini China kwa ajili ya imani yake ya Kikristo pamoja na mapadri Wadominiko wenzake Yohakim Royo, Yohane Alcober na Fransisko Diaz.[1][2]

Alitangazwa kuwa mtakatifu pamoja na wengine 119 waliofuata kifodini chake na Papa Yohane Paulo II tarehe 1 Oktoba 2000.[3]

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 28 Oktoba, lakini pamoja na wenzake ni tarehe 9 Julai[4].

  1. "Saint Francis Ferdinand de Capillas". Patron Saints Index. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2008-05-06. Iliwekwa mnamo 2008-04-24.
  2. https://www.santiebeati.it/dettaglio/92173
  3. "Den hellige Frans Fernández de Capillas (1607-1648)" (kwa Norwegian). katolsk.no. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2008-02-09. Iliwekwa mnamo 2009-04-24. {{cite web}}: Unknown parameter |deadurl= ignored (|url-status= suggested) (help)CS1 maint: unrecognized language (link)
  4. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne