Fransisko Diaz, O.P. (Ecija, 2 Oktoba 1713 – Fuzhou, 28 Oktoba 1748) alikuwa padri kutoka Hispania aliyefanya umisionari barani Asia akauawa nchini China kwa ajili ya imani yake ya Kikristo pamoja na mapadri Wadominiko wenzake Fransisko Serrano, Yohakim Royo na Yohane Alcober.[1][2]
Alitangazwa kuwa mtakatifu pamoja na wengine 119 waliofuata kifodini chake na Papa Yohane Paulo II tarehe 1 Oktoba 2000.[3]
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake, lakini pamoja na wenzake ni tarehe 9 Julai.
{{cite web}}
: Unknown parameter |deadurl=
ignored (|url-status=
suggested) (help)CS1 maint: unrecognized language (link)