Galileo Galilei

Galileo Galilei alivyochorwa.

Galileo Galilei (5 Februari 15648 Januari 1642) alikuwa mtaalamu wa fizikia, hisabati na astronomia kutoka nchini Italia.

Anakumbukwa kwa sababu aliweka misingi ya mbinu mpya za sayansi zinazoendelea kutumika hadi leo. Akiwa mtaalamu wa kwanza aliyetumia darubini kwa kutazama nyota na sayari na kwa njia hiyo alipanua ujuzi wa binadamu juu ya ulimwengu.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne