Galus I wa Clermont

Galus I wa Clermont (Clermont-Ferrand, leo nchini Ufaransa, 489 hivi - Clermont-Ferrand, 553 hivi) alikuwa askofu wa 16 wa mji huo kuanzia mwaka 527 hadi kifo chake[1].

Mtoto wa makabaila, alikataa ndoa akawa mmonaki mnyenyekevu na mpole. Kwanza alifanywa padri, halafu askofu, akaongoza kwa ufanisi mkubwa[2], kama ilivyoandikwa na Gregori wa Tours, aliyekuwa mwanafunzi wake na mwana wa ndugu yake.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 14 Mei[3].

  1. http://www.santiebeati.it/dettaglio/53140
  2. Jones, Terry. "Gall". Patron Saints Index. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2007-11-09. Iliwekwa mnamo 2007-11-09.
  3. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne