Jamhuri ya Ghana | |
---|---|
Kaulimbiu: Freedom and Justice (Kiingereza) "Uhuru na Haki" | |
Wimbo wa taifa: God Bless Our Homeland Ghana "Mungu Ibariki Nchi Yetu Ghana" | |
Mji mkuu na mkubwa | Accra |
Lugha rasmi | Kiingereza |
Eneo | |
• Jumla | km2 238 533[1] |
Idadi ya watu | |
• Kadirio la 2023 | 33 846 114[1] |
Ghana, kirasmi Jamhuri ya Ghana, ni nchi ya Afrika Magharibi inayopakana na Kodivaa upande wa magharibi, Burkina Faso upande wa kaskazini, Togo upande wa mashariki, na Ghuba ya Guinea upande wa kusini.
Kabla ya ukoloni Ghana ilikaliwa na idadi ya watu wa kale, hasa wa Falme za Akan, wakiwemo Waakwamu upande wa mashariki, Ufalme wa Ashanti ya bara na falme kadha wa kadha za Kifante, pia falme zisizo za Kiakan kama Waga na Waewe waliokuwa pwani na bara.
Biashara na nchi za Ulaya ilistawi baada ya kukutana kwao na Wareno katika karne ya 15, na Waingereza walianzisha nchi ya Gold Coast, chini ya himaya ya Uingereza mwaka wa 1874.[2]
Nchi ya Gold Coast ilijinyakulia uhuru kutoka kwa Uingereza mwaka wa 1957, ikawa taifa la kwanza la Afrika Kusini mwa Sahara kufanya hivyo[3][4][5]
Ghana ni mwanachama wa mashirika mbalimbali ya kimataifa yakiwemo Jumuiya ya Madola, Jumuiya ya Kiuchumi ya Afrika Magharibi, Umoja wa Afrika, na Umoja wa Mataifa.
Ghana ni nchi ya pili baina ya nchi zinazozalisha mmea wa kakao ulimwenguni kote, pia ni kiambo cha Ziwa Volta, ambalo ndilo ziwa kubwa zaidi ulimwenguni kuundwa na binadamu[6].
Vilevile, Ghana ni nchi inayojulikana sana katika ulimwengu wa soka. Tarehe 16 Oktoba 2009, Ghana lilikuwa taifa la kwanza la Kiafrika kushinda Kombe la Dunia la FIFA kwa walio chini ya umri wa miaka 20 (FIFA U-20 World Cup) kwa kushinda nchi ya Brazil kwa mabao 4 kwa 3 kupitia mikwaju ya penalti[7].
{{cite web}}
: CS1 maint: date auto-translated (link) (Archived 2023 edition)
{{cite web}}
: Unknown parameter |=
ignored (help); Unknown parameter |deadurl=
ignored (|url-status=
suggested) (help); Unknown parameter |https://www.webcitation.org/5kwptUKKy?url=
ignored (help)