Gideoni

Gideoni alivyochorwa na Maarten van Heemskerck (1550 hivi).

Gideoni (kwa Kiebrania גדעון - Ghide'on) alikuwa mwana wa Yoas, wa kabila la Manase.

Mungu alimuita awe mwamuzi wa Israeli kwa miaka 40; kisha kupewa ishara ya umande kwenye ngozi iliyotandazwa ardhini, kwa nguvu ya Mungu alibomoa altare ya Baal akakomboa sehemu kubwa ya nchi kutoka mikono ya Wamidiani kama kitabu cha Waamuzi (6-8) kinavyosimulia[1].

Kwa jinsi anavyosifiwa na Waraka kwa Waebrania, anaheshimiwa katika imani ya Wakristo wote ulimwenguni kama mtakatifu kulingana na ushuhuda wake katika kipindi chake cha kuwa mwamuzi wa Israeli.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 26 Septemba[2].

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/92462
  2. Martyrologium Romanum

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne