Godfrey Mwakikagile

Godfrey Mwakikagile

Godfrey Mwakikagile (alizaliwa Kigoma, 4 Oktoba 1949) ni mwandishi Mtanzania aishiye nchini Marekani. Anajulikana hasa kwa kuandika wasifu wa rais Julius Kambarage Nyerere.

Ameandika zaidi ya vitabu sabini [1]. Vitabu vyake vingi vinatumiwa vyuoni katika nchi mbalimbali duniani. Ameandika vitabu vya siasa, uchumi, historia na masomo mengine kuhusu bara la Afrika na nchi mbalimbali katika bara hilo. Pia ameandika vitabu kuhusu watu weusi wenye asili ya Kiafrika nchini Marekani, Uingereza na visiwa vya Karibi pamoja na nchi ya Belize, bara la Amerika, ambayo pia ina asili ya watumwa kutoka Afrika.

Pia aliwahi kuwa mwandishi wa gazeti la Daily News ambapo wakati huo lifahamika kama "The Standard".

Mwakikagile alikuja kupata umaarufu baada ya kuandika kitabu kinachoitwa Nyerere and Africa: End of an Era [2], ambacho ni biografia ya Rais wa kwanza wa Tanzania Julius Nyerere na ambacho kinaongelea Afrika, maisha ya ukoloni, vita vya ukombozi katika nchi za kusini mwa Afrika ambapo Nyerere alisaidia kwa kiasi kikubwa.

  1. "Godfrey Mwakikagile Books | List of books by author Godfrey Mwakikagile". ThriftBooks. Iliwekwa mnamo 22 Nov 2022.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  2. Mwakikagile, Godfrey (22 Nov 2007). "Nyerere and Africa: End of an Era". New Africa Press. Iliwekwa mnamo 22 Nov 2022 – kutoka Google Books.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne