Goliathi (kwa Kiebrania גָּלְיָת, Golyat; kwa Kiarabu جالوت , Ǧulyāt) alikuwa jitu[1] la kabila la Wafilisti ambaye habari zake zinasimuliwa na Biblia na Kurani.
Kitabu cha Kwanza cha Samueli sura ya 17 kinasema kijana Daudi alishindana naye akitumia kombeo na mawe akafaulu kumshinda na kumuua. Habari hii ya kusisimua imejulikana sana ikileta ujumbe wa kwamba wasio na uwezo wa kwao kwa nia imara na kwa msaada wa Mungu wanaweza kushinda wanaowazidi.
Hata hivyo Kitabu cha Pili cha Samueli 21:19 kinamtaja Elhanan bin Jair kama muuaji wa Goliathi[2]. Tofauti hiyo inatokana na jinsi vitabu hivyo viwili vilivyotungwa kwa kukusanya mapokeo yoyote juu ya mwanzo wa Ufalme wa Israeli bila kuyachambua[3].
Goliathi anatajwa pia katika Qur'an (2: 247–252)[4].
{{cite journal}}
: CS1 maint: date auto-translated (link)