Gregori wa Nazianzo (Arianzo, leo Güzelyurt nchini Uturuki, 329 - Arianzo, 25 Januari 390) alikuwa askofu, mwanateolojia na mwanashairi maarufu kutoka katikati ya nchi ambayo leo inaitwa Uturuki.
Tangu zamani anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Waorthodoksi, halafu na Waanglikana kama mtakatifu na mmojawapo kati ya mababu wa Kanisa muhimu zaidi.
Kwa Wakatoliki ni pia (tangu 1568, alipotangazwa na Papa Pius V) mwalimu wa Kanisa.
Sikukuu yake inaadhimishwa mwezi Januari tarehe 2[1], 25 au 30, kadiri ya madhehebu.