Abu Abdullah Muhammad Ibn Battuta (kwa Kiarabu: أبو عبد الله محمد بن بطوطة) alikuwa mpelelezi na mtaalamu Mwarabu wa karne ya 14. Kwa usafiri mgumu wa siku zile alitembelea nchi mbalimbali na kuvuka umbali mkubwa kushinda mtu yeyote wa siku zile anayejulikana. Kutoka kwake tunayo taarifa ya kwanza kuhusu mji wa Kilwa Kisiwani.