Ivan Dias

Ivan Dias

Ivan Cornelius Dias (14 Aprili 193619 Juni 2017) alikuwa kardinali kutoka India katika Kanisa Katoliki.

Alitumikia kama Mkuu wa Idara ya Uinjilishaji wa Watu (Congregation for the Evangelization of Peoples) kuanzia mwaka 2006 hadi 2011, Askofu Mkuu wa Bombay kutoka 1996 hadi 2006, na kabla ya hapo alikuwa balozi wa papa katika maeneo ya Balkani, Asia ya Mashariki, na Afrika Magharibi.

Dias alipandishwa hadhi kuwa kardinali mwaka 2001.[1]

  1. "Indian Cardinal Ivan Cornelius Dias dies – UCA News". ucanews.com (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2020-06-04.

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne