Jenasi

Ngazi za uainishaji katika biolojia; ngazi ndogo za kati hazionyeshwi

Jenasi (kutoka Kigiriki Γένος genos / Kilatini genus "nasaba, ukoo, familia, aina")[1] ni ngazi katika uainishaji wa kisayansi unaopanga viumbehai (mimea, wanyama) katika vikundi kulingana na nasaba zao.

Jenasi moja huwa na spishi ndani yake. Jenasi kwa pamoja hupangwa katika familia.

Katika jina la Kisayansi la kiumbehai ni lazima kutaja jenasi. Kwa mfano paka anaitwa "Felis silvestris catus". Felis ni jina la jenasi. Jenasi huandikwa kwa herufi kubwa.

  1. kwa uwingi wa jenasi kuna pia neno "jenera" ambayo ni uwingi wa Kilatini unaotumiwa pia kwa Kiingereza

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne