Juliani wa Sora

Juliani wa Sora (alifariki Sora, Lazio, Italia, 161 hivi) alikuwa Mkristo aliyeuawa kwa kukatwa kichwa wakati wa dhuluma ya kaisari Antoninus Pius dhidi ya imani hiyo kwa kuwa alihubiri Injili akitokea Dalmatia (leo nchini Kroatia) na kuelekea Campania[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu mfiadini.

Wa kwanza wanaadhimisha sikukuu yake tarehe 27 Januari[2], wa pili tarehe 11 Agosti[3].

  1. St. Julian of Sora Catholic Online
  2. Martyrologium Romanum
  3. "The Holy Martyr Julian. Commemorated July 28 (Civil Date: August 11 )". www.orthodox.net (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2017-03-01.

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne