Jumamosi ni siku ya saba katika juma (wiki) ya siku saba yenye asili ya kiyahudi-kikristo. Iko kati ya siku za Ijumaa na Jumapili. Katika hesabu ya kimataifa ya ISO 8601 ni siku ya sita.
Katika kawaida ya utamaduni wa magharibi Jumamosi imekuwa siku ya kuanza wikendi ikiwa ni siku ambako wafanyakazi wengi hupunzika au hufanya kazi nusu siku tu.
Katika Israeli Jumamosi huheshimiwa kama Sabato ya kibiblia. Wikendi ya Israel inaanza siku ya Ijumaa na kuendelea Jumamosi.