| |||||
Kaulimbiu ya taifa: -- | |||||
Wimbo wa taifa: La Marseillaise | |||||
Mji mkuu | Nouméa | ||||
Mji mkubwa nchini | Nouméa | ||||
Lugha rasmi | Kifaransa | ||||
Serikali | (Eneo la ng'ambo la Ufaransa) Emmanuel Macron Thierry Lataste Philippe Germain | ||||
Eneo la ng'ambo la Ufaransa {{{established_events}}} |
{{{established_dates}}} | ||||
Eneo - Jumla - Maji (%) |
18,575 km² (ya 154) -- | ||||
Idadi ya watu - [[]] kadirio - Agosti 2014 sensa - Msongamano wa watu |
(ya 182) 268,767 14.5/km² (ya 200) | ||||
Fedha | CFP franc (XPF )
| ||||
Saa za eneo - Kiangazi (DST) |
(UTC+11) (UTC) | ||||
Intaneti TLD | .nc | ||||
Kodi ya simu | +687
- |
Kaledonia Mpya (kwa Kifaransa: Nouvelle-Calédonie - nuvel kaledoni) ni eneo la ng'ambo la Ufaransa katika bahari ya Pasifiki.
Kisiwa kikubwa cha Grande Terre pamoja na visiwa vingine ni sehemu ya Melanesia.
Jumla ya eneo la visiwa vyote ni km² 18,575.
Wakazi ni 268,767 (sensa ya mwaka 2014). Kati yao, 39.1% ni Wakanaki, ambao ni wa jamii ya Wamelanesia na ndio wakazi asili wa visiwa hivyo. Walau 30% ni Wazungu, wengine wana asili ya Polinesia na Asia Kusini Mashariki.
Kifaransa ndiyo lugha inayotumika zaidi.
Upande wa dini, karibu wote ni Wakristo: 50% ni Wakatoliki, wengine Waprotestanti.
Hadi sasa pesa ni Franc ya pasifiki lakini kuna majadiliano kutumia Euro jinsi ilivyo kwa Ufaransa bara.
Watu wa Kaledonia Mpya wamepiga kura tarehe 4 Novemba 2018 na 56.40% wamependelea kuendelea kuwa sehemu ya Ufaransa, si kujitegemea kama nchi huru.