Kanisa la Anglikana la Tanzania


Kanisa Anglikana la Tanzania ( ACT ) ni jimbo la Jumuiya Anglikana Duniani. Makao makuu yake yako Dodoma. Lina dayosisi 28 ambazo ziko 27 Tanzania bara na 1 iko Zanzibar. Kila dayosisi huongozwa na askofu wake.

Hadi mwaka 1970, Waanglikana wa Tanzania walikuwa sehemu ya Jimbo la Afrika ya Mashariki pamoja na Kenya hadi kuanzishwa kwa majimbo ya pekee kila upande.

Askofu Mkuu wa Kanisa Anglikana Tanzania tangu mwaka 2018 ni Maimbo Mndolwa. [1]

  1. "I will be Maimbo" - New Primate of Tanzania honours past as he ushers in new era, Anglican Communion News Service, 21 May 2018

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne