Karafuu (kutoka Kiarabu قَرَنْفُل qaranful[1]) ni matumba (macho ya maua) makavu ya mikarafuu ambayo ni miti ya familia ya Myrtaceae.
Karafuu hutumiwa kama kiungo cha chakula na chanzo cha mafuta yenye harufu inayopendwa na watu wengi.
Asili ya mti na pia matumizi ya matumba ni visiwa vya Indonesia. Katika karne ya 19 mikarafuu ilipelekwa Unguja na Pemba hasa na mtawala wa Omani na kuanzisha uzalishaji mkubwa saa wa karafuu kwenye visiwa hivi.