Kaunti ya Mombasa Kaunti 001 | |||||
---|---|---|---|---|---|
Kaunti | |||||
| |||||
Kaulimbiu: "Utangamano kwa maendeleo" | |||||
Mombasa County in Kenya.svg![]() Kaunti ya Mombasa katika Kenya | |||||
Coordinates: 4°03′S 39°40′E / 4.050°S 39.667°E | |||||
Nchi | ![]() | ||||
Nambari | 1 | ||||
Ilianzishwa | Tarehe 4 Machi, 2013 | ||||
Ilitanguliwa na | Mkoa wa Pwani | ||||
Mji mkuu | Mombasa | ||||
Miji mingine | |||||
Serikali | |||||
Gavana | Hassan Ali Joho | ||||
Naibu wa Gavana | Dkt. William Kingi | ||||
Seneta | Mohammed Faki | ||||
Mwakilishi wa wanawake | Asha Hussein Mohammed | ||||
Bunge | Bunge la Kaunti ya Mombasa | ||||
Spika | Arub Ibrahim Khatri | ||||
Wawakilishi Wadi | 30 | ||||
Mahakama | Mahakama ya Rufaa, Mombasa | ||||
Maeneo bunge | 6 | ||||
Eneo | |||||
Jumla | km2 219.9 (sq mi 84.9) | ||||
Idadi ya Watu | |||||
Jumla | 1,208,333 | ||||
Msongamano | 5,495 | ||||
Majira ya Saa | Saa za Afrika Mashariki (UTC+3) | ||||
Tovuti mombasa.go.ke |
Kaunti ya Mombasa imeshika nafasi ya wilaya ya Mombasa baada ya katiba mpya ya Jamhuri ya Kenya kupatikana mwaka 2010. Kaunti hii ni mojawapo ya kaunti mbili ambazo pia ni jiji na ndio kaunti ndogo kabisa kati ya kaunti zote.
Inapakana na kaunti za Kwale na Kilifi ambazo pamoja na kaunti za Mombasa, Lamu, Tana River na Taita Taveta zilikuwa zinatengeneza Mkoa wa Pwani.
Wakati wa sensa ya mwaka 2019 wakazi walikuwa 1,208,333 katika eneo la km2 219.9, msongamano ukiwa hivyo wa 5,495 kwa kilometa mraba[1].
Makao makuu ya serikali ya kaunti yako katika jiji la Mombasa.