Kialune

Kialune (pia Kisapalewa) ni lugha ya Kiaustronesia nchini Indonesia inayozungumzwa na Waalune kwenye kisiwa cha Seram. Mwaka wa 2000 idadi ya wasemaji wa Kialune imehesabiwa kuwa watu 17,200. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kialune iko katika kundi la Kimaluku. Inawezekana kuwa lugha ya Kikawe ni lahaja ya Kialune.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne