Kilifi

Kilifi
Kilifi is located in Kenya
Kilifi
Kilifi

Mahali pa mji wa Kilifi katika Kenya

Majiranukta: 3°38′0″S 39°51′0″E / 3.63333°S 39.85000°E / -3.63333; 39.85000
Nchi Kenya
Kaunti Kilifi
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 122,899
Kilifi, Kenya
Madau kwenye kihori cha Kilifi Creek

Kilifi ni mji kwenye pwani ya kusini ya Kenya uliopo kati ya Mombasa na Malindi. Iko kando ya kihori cha Kilifi ("Kilifi Creek") kinachoishia katika Bahari Hindi.

Mji ni makao makuu ya Kaunti ya Kilifi.

Wakati wa sensa ya mwaka 2009 Kilifi ilikuwa na wakazi 122,899 [1].

Kilifi imekuwa kitovu kimojawapo cha utalii nchini Kenya hasa kutokana na fuko zake za kupendeza na Bofa Beach ni marufuku hasa. Mdomo mpana wa kihori unapendwa na wenye jahazi za burudani, hivyo kuna jahazi nyingi zinazolala hapa.

  1. Sensa ya Kenya 2009 Ilihifadhiwa 9 Januari 2019 kwenye Wayback Machine., tovuti ya KNBS, ilitazamwa Januari 2009.

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne