Kisiwa cha Ukerewe

2°01′45″S 33°00′35″E / 2.029300°S 33.009796°E / -2.029300; 33.009796

Ukerewe kusini mashariki mwa Ziwa Viktoria.

Kisiwa cha Ukerewe ndicho kisiwa kikuu cha Tanzania ambacho kinapatikana katika Ziwa Viktoria, kiasi kwamba hilo linaitwa pia "Ziwa Ukerewe". Wenyeji wanakiita "Bukerebe".

Kikiwa na eneo la Km² 530 hivi, ndicho pia kisiwa kikuu cha Afrika kisicho cha baharini na kisiwa cha ziwani cha pili duniani kwa ukubwa.

Pamoja na visiwa vya jirani kinaunda Wilaya ya Ukerewe katika Mkoa wa Mwanza.

Wakazi wake ni 345,147.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne