Kitabu cha Hosea

Hosea na mke wake Gomeri katika Bible Historiale, 1372.

Kitabu cha Hosea ni kimojawapo kati ya vitabu vya Tanakh (yaani Biblia ya Kiebrania), na hivyo pia vya Agano la Kale katika Biblia ya Kikristo.

Kwa kuwa kina sura 14 tu, kimepangwa tangu zamani za kale kati ya vitabu 12 vya Manabii Wadogo.

Hata hivyo umuhimu wake katika maendeleo ya Ufunuo wa Mungu kwa Israeli ni mkubwa, kwa jinsi kilivyoathiri vitabu vilivyofuata hadi Kitabu cha Ufunuo.

Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo hayo.


From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne