Kitabu cha Ruthu ni kimojawapo kati ya vitabu vifupi vya Biblia ya Kiebrania, kwa hiyo pia ya Agano la Kale katika Biblia ya Kikristo.
Ni kati ya vile vichache vilivyo na jina la mwanamke ambaye ndiye mhusika mkuu wa habari.
Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.