Kitabu cha Yobu (kinaitwa pia Ayubu) ni kati ya vitabu vya hekima katika Biblia ya Kiebrania (Tanakh), hivyo pia cha Agano la Kale ya Biblia ya Kikristo.
Miongoni mwa aina nyingi za vitabu vya Biblia vipo hivyo vinavyojulikana kuwa vitabu vya hekima. Kati ya vitabu hivyo, pamoja na Yobu, kuna Methali na Mhubiri, ingawa hata baadhi ya Zaburi na sehemu za vitabu vingine pia vinaweza kuhesabiwa kuwa ni maandiko ya hekima. Tena, kati ya Deuterokanoni, vingi ni vitabu vya hekima.