Kizazi cha dhahabu cha hip hop

Run-DMC na Beastie Boys katika picha ya vyombo vya habari iliyotolewa kwa ajili ya ziara yao ya Together Forever mwaka 1987.

Kizazi cha dhahabu cha hip hop ni jina la kutaja enzi ya dhahabu katika anga la muziki wa hip hop ulioundwa katikati au mwishoni mwa miaka ya 1980—hadi mwanzoni au katikati mwa miaka ya 1990.[1] [2][3][4]Wanaotajwa kuwa miongoni mwa kizazi hiki walitokea mjini New York. Wakaipa jina la new-school, huku ikichukua sura mpya kabisa kuanzia ubora, ubunifu, na ushawishi wake katika hip hop kwa ujumla baada ya aina hiyo kujitokeza na kuimarika katika enzi ya old-school. Pia, inahusiana na maendeleo na mafanikio ya hip hop kama tasnia kuu ya muziki.

Mada zilikuwa za aina mbalimbali, huku muziki ukijaribu mitindo mipya na kutumia sampuli kutoka kwa rekodi za zamani ili kuleta mtazamo mpana na tofauti.

Wasanii wanaohesabiwa kuwa hasa ni wa kizazi hiki ni pamoja LL Cool J, Slick Rick, Ultramagnetic MC's,Jungle Brothers, Run-DMC, Public Enemy, Beastie Boys, KRS-One, DJ Jazzy Jeff & the Fresh Prince, Eric B. & Rakim, De La Soul, Big Daddy Kane, EPMD, Biz Markie, Salt-N-Pepa, Queen Latifah, Gang Starr, na A Tribe Called Quest.

Albamu na nyimbo za wasanii hawa ziliibuka sambamba na zile za wasanii wa awali wa gangsta rap kama Schoolly D, Ice-T, Geto Boys, na N.W.A, pamoja na muziki wa kimahaba wa 2 Live Crew na Too Short, pamoja na muziki wa amsha-amsha kutoka kwa wasanii kama Fat Boys, MC Hammer, na Vanilla Ice.[5][6][7]

  1. "Golden Age Music Style Overview". AllMusic (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2025-02-09.
  2. Carl Stoffers (2015-11-27). "Hip hop's golden age: Where are they now?". New York Daily News (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2025-02-09.
  3. Hess, Mickey., 2007, Icons of Hip Hop [Two Volumes] [2 volumes]: An Encyclopedia of the Movement, Music, and Culture (Greenwood Icons), Greenwood Publishing Group, p. 341.
  4. Duinker, Ben; Martin, Denis (2017-09-26). "In Search of the Golden Age Hip-Hop Sound (1986–1996)". Empirical Musicology Review (kwa Kiingereza). 12 (1–2): 80–100. doi:10.18061/emr.v12i1-2.5410. ISSN 1559-5749.
  5. Bakari Kitwana (2005-06-21). "The Cotton Club". The Village Voice (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2025-02-09.
  6. Dan Epstein (2016-10-18). "'Cool as Ice': The Story Behind Vanilla Ice's Career-Killing Movie". Rolling Stone (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2025-02-09.
  7. "www.usatoday.com - Spin magazine picks Radiohead CD as best". www.usatoday.com. Iliwekwa mnamo 2025-02-09.

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne