Klaudi wa Condat

Klaudi wa Condat

Mt. Klaudi katika dirisha la kioo cha rangi
Nchi Ufaransa
Kazi yake Mtakatifu

Klaudi wa Condat (au wa Besancon; Bracon, Jura, karibu Salins-les-Bains, Ufaransa, 607 hivi - 6 Juni 696 au 699) alikuwa padri, halafu mmonaki aliyepata kuwa abati wa Condat na hatimaye askofu wa Besancon, maarufu kwa miujiza[1][2].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 6 Juni[3].

  1. Saint-Claude (Municipality, Jura, France)
  2. http://www.santiebeati.it/dettaglio/56090
  3. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Nelliwinne