Kristine Hermosa | |
---|---|
![]() Kristine Hermosa akiwa katika Tamasha la Ziara ya Star Magic huko mjini Ontario mnamo Juni 2009. | |
Amezaliwa | Kristine Hermosa Orille 9 Septemba 1983 |
Utaifa | Hispania/Ufilipino |
Asili yake | Masbate, Ufilipino |
Kazi yake | Mwigizaji, mwanamitindo |
Miaka ya kazi | 1996–2011; 2016–hadi sasa |
Wakala | Star Magic (1996-2010) GMA Artist Center (2016-hadi sasa) |
Anajulikana kwa ajili ya | Pangako Sa 'Yo Sana'y Wala Nang Wakas Dahil May Isang Ikaw |
Ndoa | Diether Ocampo (m. 2004–2005) Oyo Sotto (m. 2011–present) |
Watoto | 3 |
Kristine Hermosa Orille (Amezaliwa tar. 9 Septemba 1983 mjini Quezon City, Ufilipino) ni mwigizaji maarufu kutoka nchi Ufilipino. Hermosa alizaliwa na matabaka mawili, mama yake ni mwispania , baba yake ni mfilino.
Hermosa pia ana dada yake aitwae Kathleen, ambaye aliyekuwa na shauku ya kuwa nyota wa ‘’ABS-CBN’’. Ingawaje, dada yake Hermosa alifeli kumvutia mwamuzi katika uchgauzi wa kwanza wa wasanii, badala yake akachaguliwa mdogo wake mrembo mwenye sura ya kuvutia iliopelekea mwamuzi kumchagua, ni Kristine Hermosa, aliyechaguliwa kuwa msanii wa ‘’ABS-CBN’’.
Ilifikiriwa kuwa ni msanii mwingine tena mdogo mwenye urembo safi, aliyepatia umaarufu wake katika tamthlia ya "Pangako Sa 'Yo" (Kwa kiing The Promise) ambayo ndio iliomjengea umaarufu mkubwa sana kwa kuigiza kama mpenzi wake Angelo Buenavista (Jericho Rosales) ambaye baadae alikua kuwa mpenzi wake wa kweli wa katika maishani.
Miaka ya mwanzo kabla Kristine kuwa maarufu, aligiiza kama Baron Geisler katika tamhilia ya Nagbibinata. Baadae, alishriki katika mchezo mmoja wa kuigiza uliojulikana kwa jina la "Sa Sandaling Kailangan Mo Ako", mchezo huo ulikuwa ukionyesha kila siku za wiki, huku akiwa sambamba kabisa na mwigizaji mwenzake bwana Marvin Agustin.